Mkutano mkuu wa jumuiya ya Watanzania, Roma, Italia.
Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Roma unapenda kuwajulisha
Watanzania wa Roma na sehemu mbali mbali za Italia kuwa, siku ya jumamosi
tarehe 22 Juni 2013, kutakuwa na mkutano mkuu wa jumuiya kwenye ukumbi wa
Wakenya Pub, uliopo kwenye mtaa wa Via Giovanni Lanza, karibu sana na Stazione
Termini kuanzia saa kumi jioni.
Agenda ya mkutano huu ni kujadiliana kwa pamoja
mwenendo mzima wa Jumuiya. Kama inavyojulikana na wote jumuiya inaitaji muamko
mkubwa kutoka kwa wanajumuiya ili iweze kuendelea daima na daima.
Kwa maelezo zaidi mnaweza kuwasiliana na katibu
kwa Namba hii 3479094800.
Nawatakia siku njema.
Andrew Chole Mhella
Katibu.
No comments:
Post a Comment