Tuesday, June 11, 2013

Mkutano mkuu wa jumuiya ya Watanzania, Roma, Italia.

Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania Roma unapenda kuwajulisha Watanzania wa Roma  na sehemu mbali mbali za Italia kuwa, siku ya jumamosi tarehe 22 Juni 2013, kutakuwa na mkutano mkuu wa jumuiya kwenye ukumbi wa Wakenya Pub, uliopo kwenye mtaa wa Via Giovanni Lanza, karibu sana na Stazione Termini kuanzia saa kumi jioni.
Agenda ya mkutano huu ni kujadiliana kwa pamoja mwenendo mzima wa Jumuiya. Kama inavyojulikana na wote jumuiya inaitaji muamko mkubwa kutoka kwa wanajumuiya ili iweze kuendelea daima na daima.
Kwa maelezo zaidi mnaweza kuwasiliana na katibu kwa Namba hii 3479094800.
Nawatakia siku njema.
Andrew Chole Mhella
Katibu.TANZANIAN COMMUNITY IN ROME-ITALY( COMUNITA' TANZANIANA A ROMA)

No comments:

Post a Comment