Story
la leo inanirudisha nyuma kidogo.
Siku
moja nikiwa Tanzania, kama kawaida yangu kufuatilia habari, nilipomaliza
kutazama ile ya TBC1, nikatupia macho Star Tv.
Hapo
nikakutana na matangazo ya BBC kwa lugha ya Kiswahili. Ilitangaz moja kwa moja kutokea
London, nchini Uingereza. Studioni nikamwona mtangazaji, Salim Kikeke akimuaga na kumkaribisha tena, kijana aliyezungumza
Kiswahili huku pembeni yake ikiwa imepaki baiskeli. Akainuka. Akaiufuata baiskeli
na kuikokota hadi nje ya studio.
Sikuwahi
kipindi tangu mwanzo,kwa hiyo sikuelewa kilichomfanya kijana yule kuwa pale akihojiwa.
Haraka haraka, nikajiamninisha kwambaa pengine ni mmoja kati ya washiriki wa
mbio za kukimbizana kwa baiskeli na ile ilikuwa ni habari ya michezo!
Ila
wakati maswali yananizidi uwezo, mdogo wangu aliyeifuatilia pia habari ile,
akaniuliza,
“Mbona
kama unashangaa bro, kulikoni? Au unamshangaa Lelo?”
“Lelo?”
Nikamjibu kwa kumuuliza swali. “Lelo ni nani?”
“Ni yule kijana uliyemwona anatoka na baiskeli
pale!” akajibu na kuinuka. Akatokomoe huyo, chumbani.
Nikabaki
mbele ya Tv peke yangu. Nilitaman kuendela kumwuliza ili anijuze mengi. Kiu ya
haki ya ufahamu, ilishanikaba. Mara huyo. Anarudi kutoka chumbani. Mikono
yake,imejaa laptop yake.
“Soma
mtandao huu, niliufuatilia tangu jana!”
“Nilipoutazama
nikakukana na www.chiletokili.com”
Nikagundua
safari ya maajabu!
Anaitwa
Elvis Munisi, a.k.a Lelo, mzaliwa wa Tanzania. Ameamua kuzunguka dunia nzima kwa kutumia
baiskeli yake, kutokea nchini Chile hadi mlima Kilimanjaro.
Lengo
lake kuu, sio kutalii, bali ni kuchangisha pesa kwa ajli ya masomo ya mambo ya mazingira.Usiku mzima nililala nikimfikiria Elvisi na kukumbuka maneno mengi ya wanafalsafa akiwemo Mahatma Gandhi aliyesema, “Be The Change You Want To See In The World’’ akimaansiha kwamba kuwa chanzo cha mabadliko kwa namna unavyoona dunia inapaswa iwe.
Elvis Munis pichani.
Inabidi apigiwe makofi..napenda kutembelea baiskeli lakini huyu kiboko. Hongera na kila la heri
ReplyDeleteJambo alilofanya ni kubwa na la ajabu sana! Zaidi ya kupigiwa makofi, nadhani anafaa pia kuwekwa kwenye vitabu vya kumbukumbu za rekodi ya dunia!
Delete